Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Fahyvanny aanika mazito kuhusu Rayvanny
Michezo

Fahyvanny aanika mazito kuhusu Rayvanny

Spread the love

 

MWANAMITINDO na mzazi mwenza wa Staa wa Bongofleva, Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’, Faima Msenga ‘Fahyma au Fahyvanny’ ameweka wazi kuwa hana matatizo na baba wa mtoto wake kwa kuwa anawahudumia vizuri yeye na mwanaye. Anaripoti Matilda Buguye, Dar es Salaam … (endelea).

Mwanamitindo huyo amefunguka hayo leo tarehe 30 Septemba, 2021 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kuhusu ubalozi wa vipodozi kutoka La vista organic product.

Fahyvanny ambaye amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kuachana na Rayvanny, amesema anamheshimu sana msanii huyo ambaye ni CEO wa lebo ya Next Level Music.

“Mtoto wetu hakuna anachokikosa kwa sababu kwanza anatuona wote wawili… siwezi kuzungumzia kwa kina zaidi kwa sababu haya ni masuala ya kifamilia,” amesema Fahyma.

Aidha, akizungumzia sababu za kutobadilisha jina analolitumia kwenye mtandao wake wa Instagram linalounganisha jina lake na Rayvanny yaani (Fahyvanny), amesema jina hilo limehalalishwa na mtandao huo kwa hiyo ni ngumu kulibadilisha

“Hata kama nikibadilisha jina itakuwa haina maana yeyote kwani nitaonekana mimi nina matatizo, lakini sisi tuko poa na hatuna shida yoyote pia tuna mawasiliano mazuri kama wazazi,” amesema.

Aidha, Mwanamitindo huyo amekanusha sauti zilizozagaa mitandaoni wiki kadhaa zilizopita zikisikika kumuagiza dereva wa bodaboda amfuatilie mpenzi wa sasa wa mzazi mwenzie Rayvanny, Paula ambaye wapo kwenye mahaba mazito.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!