Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Tizeba aibua shangwe bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Tizeba aibua shangwe bungeni

Aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba
Spread the love

MBUNGE wa Buchosha, Dk. Charles Tizeba aliyekuwa Waziri wa Kilimo ameibua shangwe bungeni kwa kushangiliwa na wabunge aliposimama kwa ajili ya kuuliza swali la nyongeza. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dk. Tizeba aliyevuliwa wadhifa wa uwaziri wa kilimo na Rais John Magufuli tarehe 10 Novemba 2018 na nafasi yake kuchukuliwa na Japhet Hasunga, kwa mara ya kwanza leo tarehe 13 Novemba 2018 alisimama bungeni kama mbunge wa kawaida.

Aliposimama kwa ajili ya kuuliza swali, alianza kwa kumshukuru Rais Magufuli kwa fursa aliyompa ya kuwa waziri pamoja na kuushukuru uongozi wa bunge kwa ushirikiano alioupata wakati akiwa kwenye wadhifa huo, ndipo wabunge walizidisha kumshangilia kwa kupiga makofi.

Katika swali lake la nyongeza, Dk. Tizeba alihoji kama serikali inaendelea na dhamira yake ya kujenga vivuko vipya kutokana na jimbo lake lenye visiwa takribani 28 kuwa na uhaba wa vivuko, kitendo iinachohjatarisha usalama wa wananchi wa jimbo hilo.

“Jimbo langu la Buchosa linavyo visiwa zaidi ya 28 kuna vivuko viwili, kimoja kimepitwa na wakati kinakuwa ‘overloaded’ kinaelemewa na mizigo, wakati mwingine watu wanaogopa kupanda, je comitment (dhamira) ya kujenga kivuko kipya iko pale pale au lah,” amehoji Dk. Tizeba.

Akijibu swali hilo,Naibu Waziri Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Elias Kuandikwa amesema utaratibu wa kuboresha usafiri katika jimbo hilo unaendelea na kwamba serikali imeunda timu ya kutembelea vivuko vilivyopo, kisha kurekebisha kivuko kilichoharibika .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!