BALOZI Dk. Willibroad Slaa leo Ijumaa amesema kitendo cha polisi kumkamata kinguvu tarehe 13 Agosti 2023 kisha kutuhumiwa kwa uhaini, hakitamrejesha nyuma katika jitihada zake za kutetea rasilimali za Taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Akizungumza nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam baada ya kuachiwa kwa dhamana amesema; “Wasifikirie kitendo cha kunichukua siki ile kwa nguvu kama kitanirejesha nyuma kushiriki na watanzania wenzangu kujadili rasilimali zetu sitarudi nyuma.
“Ninachojua nimetimiza wajibu wangu wa kikatiba ya kupiga kelele juu ya rasilimali kama ni kosa basi hatuna Katiba itakuwa ni karatasi tu…sitashaanga Katiba hii kuvunjwa kwani imekuwa ikivunjwa kila siku,” amesema na kuongeza;
“Kama Bunge halisemi haya sisi tutayasemea …kama wabunge tuliowachagua hawatekelezi wajibu wao hata wakituita wachochezi kama kutuweka jela watuweke tu. Afadhali uhukumiwe duniani kuliko kuhukumiwa mbinguni.”
Leave a comment