WAKILI Dickson Matata amethibitisha kuwa Balozi Dk. Wilbroad Slaa amerejeshwa Dar es Salaam na kutakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho kutoka kata wanazoishi ili aachiwe kwa dhamana.
Hatua hiyo inakuja baada ya usiku wa jana Alhamisi kusafirishwa kutoka Mbeya na kuletwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay -Dar es Salaam.
Akizungumza na MwanaHALISI online leo Ijumaa Wakili Matata amesema amepigiwa simu na Maofisa wa Polisi wa kituo hicho na kumtaka afike kwa ajili ya utaratibu wa dhamana ya Dk. Slaa.
“Polisi wametaka wadhamini wawili wenye barua za utambulisho kutoka kata wanazoishi. Nipo kwenye mchakato wa kisheria kukamilisha taratibu hizo,” amesema.
Leave a comment