Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Shein: Nimefanikiwa
Habari za Siasa

Dk. Shein: Nimefanikiwa

Dk. Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amesema, anaondoka madarakani huku akifanikiwa kuacha visiwa hivyo (Unguja na Pemba) vikiwa na amani. Anaandika Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Akizungumza wakati wa kuaga watumishi wa serikali aliyokua akiongoza tangu mwaka 2010, amewataka kuendelea kukichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuendeleza amani hiyo.

“Naondoka madarakani nikiiacha nchi yenye amani. Ninaondoka madarakani huku nikiwa nimeacha milango yangu ya ushauri wazi kwa anayetaka kuja, lakini ajitahadhari sitaki majungu na fitina,” amesema Dk. Shein.

Amesema, katika maisha yake ametumikia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 51 na kwamba, katika utawala wake Zanzibar, amefanikiwa kujenga misingi mizuri ya uongozi, utawala bora, maendeleo.

“Namaliza muda wa utumishi wangu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano kwa muda wa miaka 51, nikiwa nimefanikiwa kujenga misingi mizuri ya utawala bora, naondoka nikiacha amani na utulivu vimetawala.

“Ninaondoka madarakani huku nikiwa nimepata mafanikio makubwa katika utendaji wa utumishi wa serikali ikiwamo kufanya marekebisho ya sheria katika Baraza la Wawakilishi zipatazo 128,” amesema.

Pia amempongeza Rais John Magufuli kwa kufanyakazi naye kazi kwa ushirikiano na kuwa, (Rais Magufuli) ni kiongozi mwenye uwezo mkubwa wa kubuni mambo yenye maslahi makubwa kwa Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!