Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Kaze: kupata matokeo ndani ya siku tano sio kitu rahisi
Michezo

Kaze: kupata matokeo ndani ya siku tano sio kitu rahisi

Cedric Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga
Spread the love

BAADA ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania kocha wa klabu ya Yanga, Cedric Kaze amesema kupata matokeo ndani ya siku tano sio kitu rahisi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa kocha huyo ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara toka alipojiunga na timu hiyo wiki iliyopita.

Kaze amesema kuwa ameona mabadiliko kwenye kikosi chake ndani ya muda mfupi licha ya mwanzo wa mchezo wachezaji wake walikuwa wanapoteza pasi kirahisi.

“Kupata matokeo ndani ya siku tano sio kitu chepesi, polisi ni timu nzuri na haijafungwa kirahisi kwenye ligi, kitu nilichopenda ni wachezaji wangu kucheza mwanza mpaka mwisho,” alisema kocha huyo.

 

Bao pekee la Yanga kwenye mchezo wa leo lilifungwa na kiungo wake Tunombe Mukoko dakika ya 70.

Baada ya matokeo hayo Yanga wanakwenda mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo kwa kufikisha pointi 15, huku Simba ikishuka nafasi ya tatu baada ya kupoteza dhidi ya Tanzania Prisons.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!