Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi amteua Dk. Mkuya, Nassor Mazrui
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mwinyi amteua Dk. Mkuya, Nassor Mazrui

Nassor Ahmed Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi amewaingiza kwenye baraza lake la amwaziri Dk. Saada Mkuya Salum, Nassor Ahmed Mazrui na Omar Said Shaaban. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kwenye uteuzi huo leo tarehe 3 Machi 2021, Dk. Mwinyi amemteua Dk. Mkuya kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Kwanza. Dk. Mkuya aliwahi kuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mazrui ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto huku Shaaban akiteuliwa kuwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda.

Saada Salum Mkuya

Mpaka anakwaa wadhifa huo, Mazrui ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo (Zanzibar).

Kabla ya kujiunga na ACT-Wazalendo, aliwahikuwa Waziri wa Biashara na Utalii wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar na Mjumbe wa Baraza Kuu la Wananchi (CUF).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi Wateule imeelez, kwamba wateule hao wataapishwa kesho tarehe 4 Machi 2021, saa 4 asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!