Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi amteua Dk. Mkuya, Nassor Mazrui
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mwinyi amteua Dk. Mkuya, Nassor Mazrui

Nassor Ahmed Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi amewaingiza kwenye baraza lake la amwaziri Dk. Saada Mkuya Salum, Nassor Ahmed Mazrui na Omar Said Shaaban. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kwenye uteuzi huo leo tarehe 3 Machi 2021, Dk. Mwinyi amemteua Dk. Mkuya kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Kwanza. Dk. Mkuya aliwahi kuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mazrui ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto huku Shaaban akiteuliwa kuwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda.

Saada Salum Mkuya

Mpaka anakwaa wadhifa huo, Mazrui ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo (Zanzibar).

Kabla ya kujiunga na ACT-Wazalendo, aliwahikuwa Waziri wa Biashara na Utalii wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar na Mjumbe wa Baraza Kuu la Wananchi (CUF).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi Wateule imeelez, kwamba wateule hao wataapishwa kesho tarehe 4 Machi 2021, saa 4 asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!