Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Costech yatoa milioni 50 kwa wabunifu wanawake
Habari Mchanganyiko

Costech yatoa milioni 50 kwa wabunifu wanawake

Mkurugenzi wa COSTECH, Dk. Amos Nungu
Spread the love

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknlojia (Costech) imetoa Sh milioni 50 kwa wabunifu wa wanawake watano walioshinda shindano la Buni Divaz. Anaripoti Faki Sosi … (endelea)

Shindano hilo lililowashindanisha wabunifu wanawake 35, watano kati yao waliokuwa na mawazo bora wameshinda.

Buni Divaz ni shindano lililoandaliwa na Costech kupitia kitengo cha ubunifu.

Akizungumza katika utoaji wa zawadi hizo Mkurugenzi wa tume hiyo Dk. Amos Nungu amesema mashindano hayo yemelenga kuwainua wabunifu wanawake na kuondosha fikra ya kwamba masuala ya teknolojia na Sayansi ni ya wanaume pekee.

Amesema nafasi hiyo ilikuwa mahususi kwa ajili ya wabunifu wanawake ili kuwaongezea ari wanawake kwenye ulimwengu wa ubunifu hasa wa teknolojia.

“Tumeona maeneo mengi wabunifu ni wanaume ndio wameshika hatamu, Tume tumetoa nafasi hii maalum kwa wanawake ili waonyeshe mawazo yao” amesema.

Amesema kuwa Tume hiyo haitaishia kutoa fedha tu, bali itaendelea kuwalea wabunifu hao mpaka wanafikia malengo yao.

Christina Charles Mwanzilishi wa Bionutrion Company, alisema wazo lake ni miongoni mwa mawazo bora yaliyomfanya kuibuka mshindi.

Amesema ushindi huo umemtia moyo na hamasa kwa wanawake wengine  waone umuhimu wa kushiriki masuala ya teknolojia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!