Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chongolo ateta na bodaboda, bajaji
Habari za Siasa

Chongolo ateta na bodaboda, bajaji

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo
Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amewaahidi vijana 26 wa shina la namba tano la kata Kilimani mkoani Dodoma kwamba atazungumza na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan ili awapatie bodaboda zitakazowawezesha kujikwamua kiuchumi. Anaripoti Dnason Kaijage, Dodoma … (endelea).

Chongolo ametoa kauli hiyo leo tarehe 23 Aprili, 2022 wakati akizindua na kushiriki kupiga kura katika shina hilo ambalo linaundwa na madereva bodaboda na bajaji.

Aidha, Chongolo amewapongeza vijana hao kwa uamuzi wa kuanzisha tawi hilo huku akiwasisitiza kuwa litumike kwa kazi kusudiwa si vinginevyo.

“Lengo letu muwe na makazi bora nyinyi na familia zetu hivyo, nawaahidi nitamuomba Rais Samia awachangie bodaboda hesabu ya jioni itakayopatikana ni yenu mtagawana,” alisema.

Chongolo ameagiza baadhi ya viongozi wa mkoa wa Dodoma kwenda kuangalia kama vijana hao wanakopesheka ili wawaingize kwenye mikopo ya halmashauri.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ametoa rai kwa madereva hao ambao ni vijana kutumia shina hilo vizuri.

Kuhusu mikopo kwa vijana hao, Shekimweri amewataka kuunda kikundi na kukisajili kitakachowawezesha kupata mikopo na kuahidi kuwapa kipaumbele pindi watakapokamilisha shatri hilo.

Hata hivyo, katika uchaguzi huo wa shina namba tano lililopo Kata ya Kilimani, Juma Saigwa aliibuka kidedea katika nafasi ya Mwenyekiti kwa kupata kura 45 sawa na asilimia 90 ya kura zilizopigwa.

Nafasi ya Katibu ilichukuliwa na Maxmillian Mtabekwa huku wajumbe watatu waliopatikana katika uchaguzi huo ni Liana Danford, Regina Kalindo na John Msalika.

1 Comment

  • Hawa bodaboda ni fujo vurugu mechi tu barabarani. Hawafuati sheria za matumizi ya barabara na polisi wala hawashughuliki. Hawavai kofia ngumu wanapakia mishkaki na wanakatiza na kuchomekea popote pale. Hatari kwa maisha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!