Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CHAUMMA nao wajiondoa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Habari za Siasa

CHAUMMA nao wajiondoa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chaumma
Spread the love

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea). 

Uamuzi huo umetangazwa leo tarehe 9 Novemba 2019 na Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa CHAUMMA Taifa, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam. 

Rungwe ameeleza kuwa, wamejitoa katika uchaguzi huo kwa kuwa mchakato wake ulikuwa na hila, kwa wagombea wa vyama vya upinzani.

“Tunashindwa, tunaona kwamba huu uchaguzi umetayarishwa kwa hila, kwamba wananchi wasishiriki. Tunaona kwamba uchaguzi huu umefanywa hila. Na sisi pia tunaamua hatutashiriki uchaguzi huu. Tunaomba wagombea wetu popote walipo wasishiriki,” ametangaza Rungwe.

Rungwe amesema wamefikia hatua hiyo, baada ya kuona jitihada zao za kutafuta suluhu kuhusu hujuma hizo, kugonga mwamba.

“Wanachama wote wafahamu huu uchaguzi una hila, tumekata rufaa lakini haijasaidia chochote. Kama wao ndio wanataka hivi, kwamba wale wana nguvu, wana dola, sisi hatuko tayari kupigana,” amesema Rungwe na kuongeza;

“Watanzania hatuko tayari kupigana. Hatuna tabia hiyo. Unatuzuia hatufanyi siasa. Sasa uchaguzi halali umeutangaza tumekuja kuchukua fomu, matatizo tunasumbuliwa, tumezirudisha zimekataliwa, tufanye nini.”

Rungwe amesema wananchi ambao ndio wapiga kura, wataamua la kufanya kuhusu uchaguzi.

Rungwe amesema CHAUMMA kilisimamisha wagombea zaidi ya 250, ambapo jiji la Dar es Salaam kilisimamisha wagombea 5, Morogoro (38), Iringa (30), Njombe (20) Tabora (38), Kigoma (10), Mwanza (25), Mara (40), Mtwara (7), Tanga 10 na Shinyanga (6).

CHAUMMA kinakuwa chama cha tatu kuususia uchaguzi huo, baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT- Wazalendo, kutangaza kujiondoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!