Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema watetea wabunge wasiwe ombaomba
Habari za SiasaTangulizi

Chadema watetea wabunge wasiwe ombaomba

Spread the love

VICENT Mashinji, Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amelituhumu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuvunja Katiba ya nchi na kuomba fedha kwa Serikali bila kufuata utaratibu, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mashinji amesema, Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila ameandika barua kwenda kwa Waziri Mkuu na nyingine kwa Katibu Mkuu Hazina akiomba fedha ajili ya amatumizi mbalimbali.

Serikali imeshatoa Shilingi bilioni saba kwa ajili ya Bunge, lakini huko nyuma tumeshuhudia ukiukwaji wa Katiba baada ya serikali kununua ndege, kujenzi wa kiwanda cha ndege Chato bila kufuata utaratibu.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara yetu ya 73 inasema kuwa wabunge wote wa aina zote watashika madaraka yao kwa mujibu wa katiba hii na watalipwa mshahara, posho, na malipo mengine kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

“Tatizo hapa siyo kupeleka pesa bungeni, tatizo ni kufuata utaratibu, Bunge ndilo linalopitisha bajeti iweje leo linaomba omba? Bunge limevunja ibara ya 137/3A na B kwa kuomba fedha za ziada nje ya bajeti yake iliyoidhinishwa na Bunge bila kufuata utaratibu wa kuipitisha bungeni,” ameongeza Mashinji.

Mwaka wa Fedha 2016/17 wabunge wamekuwa wakiondoka bungeni bila kulipwa stahiki zao moja ya sababu iliyosababisha Dk Kashilila kuandika barua ya kuomba pesa kwa Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!