Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waipa serikali fikra mpya
Habari za Siasa

Chadema waipa serikali fikra mpya

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani, kimeitaka serikali kuubinafsisha Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam, ili kuongeza ufanisi katika utoaji huduma. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 30 Desemba 2019 na Baraka Mwago, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani.

Mwago ameeleza kuwa, huduma zinazotolewa na mradi huo hazikidhi kiwango, na kusababisha usumbufu kwa wananchi.

Miongoni mwa adha wanayokumbana nayo watumiaji wa mradi huo, ni msongamano wa abiria vituoni na kwenye gari.

“Huu mradi wenzetu hawajajipanga. Mwendokasi wanasema wana magari 200 yamekwama bandarini lalini wanapishana na serikali kulipa kodi. Serikali ibinafsishe mradi wa mwendokasi ili wananchi wapate huduma bora,” ameshauri Mwago.

Wakati huo huo, Mwago ameishauri Serikali kukarabati miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam, ili kuondoa changamoto ya mafuriko katika jiji hilo.

Badala ya miradi hii mikubwa ambayo haina faida, fedha hii ingetumika kuikarabati miuondombinu ya Dar es Salaam. Kuboresha mifereji inayoelekea kwenye mto au baharini,” amesema Mwago.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!