Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto ala kiapo kizito uchaguzi mkuu 2020
Habari za SiasaTangulizi

Zitto ala kiapo kizito uchaguzi mkuu 2020

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT- Wazalendo, amekula kiapo kizito kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, chama hicho hakitakubali uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kunajisiwa kama ilivyokuwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, uliofanyika tarehe 29 Desemba 2019.

Akifungua uchaguzi wa ndani wa chama hicho katika Jimbo la Temeke leo tarehe 29 Desemba 2019, amesema wananchi wana hasira kwa kunyang’anywa haki yao ya kuchagua viongozi wa serilikali za mitaa.

“Chama hiki hakitakubali kuingia kwenye uchuguzi mkuu wa mwaka 2020, mpaka kikomeshe vitendo vya kuhujumu uchaguzi.

“Mchezo walioufanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ndio huo huo watakaoufanya kwenye uchaguzi mkuu iwapo hatutachukua hatua stahiki zitakazowaumiza,” amesema Zitto.

Amesema, vyama vya upinzani lazima vitoe somo “lazima tutoe somo kwa watawala juu ya kuwapa haki wananchi.”

Kiongozi huyo ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, amewambie viongozi watakaochaguliwa kwenye uchaguzi huo, kuwa tayari kuyakabili mazingira ya sasa ya siasa nchini

“Mazingira yetu ya kisiasa kwa sasa ni mabaya, mnapaswa kuwa tayari kuyakabili,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!