Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema: Kikosi kazi ilikuwa mbinu kuchelewesha Katiba Mpya
Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Kikosi kazi ilikuwa mbinu kuchelewesha Katiba Mpya

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imesema Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya kuimarisha demokrasia ya vyama vingi cha Rais Samia Suluhu, ilikuwa mbinu ya kuchelewesha mchakato wa katiba mpya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Akizungumza katika mkutano mkuu maalum wa Majimbo ya Nyamagana na Ilemela jijini Mwanza, jana tarehe 29 Desemba 2022, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, alidai kila mtu alipozungumza kuhusu ukamilishaji mchakato wa upatikanaji katiba mpya, aliambiwa asubiri matokeo ya utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi hicho.

“Watawala ili kuvuta muda na kupata kisingizio cha kuvuta muda wakaanzisha kitu kingine kikosi kazi cha rais, ikawa yeyote akizungumza mabadiliko na maboresho ya katiba, sheria na haki anaambiwa subiri matokeo ya ripoti ya kikosi kazi na baadhi wakaingia mtego wakawa na matumaini kwamba Chadema wamegoma kuingia kikosi kazi hawataki mazungumzo,”

“Hawa wanajipenda wenyewe, kumbe Chadema tuliona kuanzia mwanzo kwamba hakuna cha maana kitakachotokana na kikosi kazi, isipokuwa kuchelewesha muda wa mabadiliko katika taifa letu,” alisema Mnyika.

Mnyika alisema kuwa, kama muswada wa kurejesha, kuendeleza na kukamilisha mchakato wa katiba mpya hautapelekwa bungeni Februari 2023, haitapatikana kabla ya chaguzi zijazo, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025.

“Kama muswada huo usipoingia bungeni Februari 2023, uwezekano wa katiba mpya kukamilika na kutumika kwa ajili ya chaguzi zijazo itakuwa sawa sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano sababu hakutakuwa na bajeti ya kufanikisha mchakato huo,” alisema Mnyika.

Kikosi kazi hicho kiliundwa na Rais Samia kwa ajili ya kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na wadau kwa ajili ya kuimarisha demokrasia ya vyama vingi, ambapo kilipendekeza mchakato wa katiba mpya uanze baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!