Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema: Fedha za kurudia uchaguzi zikatibie wazee
Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Fedha za kurudia uchaguzi zikatibie wazee

Spread the love

BARAZA la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limetaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kubadilisha utaratibu wa kuwapata wabunge, katikati ya Bunge. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Jumatatu, Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Roderick Lutembeka amesema, fedha nyingi zinatumika kwenye uchaguzi, bila sababu za msingi.

Amesema, “tunaweza kuokoa mamilioni ya shilingi zinazotumika kwenye chaguzi za marudio, ikiwa tutabadilisha utaratibu wa kuwapata wabunge, katikati ya kipindi cha Bunge.”

Kwa mujibu wa Lutembeka, NEC inaweza kubadilisha utaratibu kwa kuruhusu chama ambacho mbunge wake amejiuzulu au kufariki dunia, kuteuwa mtu mwingine kushika nafasi hiyo.

“Fedha hizi zinazotumika katika chaguzi za marudio, zinapotea bure. Sisi katika Chadema, tunapendekeza zitumike kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa wazee. Tunataka ziboreshe maisha yao, badala ya umalaya wa kisiasa,” ameeleza.

Amesema, wazee nchini wanakabiliwa na matatizo makubwa, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa huduma bora za afya, madawa na wataalamu maalum wa magonjwa ya wazee.

Anasema, “…utoaji wa huduma za afya kwa wazee hauridhishi. Kuna ukosefu wa dawa na wataalamu waliojikita kuhusu masuala ya wazee. Lakini serikali inapoteza fedha katika chaguzi ambazo zinaweza kuepukika.”

Kauli ya Lutembeka inakuja katika kipindi ambacho lundo la wabunge na madiwani wa upinzani, wanavihama vyao vyao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika hatua nyingine, baraza hilo limeitaka serikali kutunga sheria ya wazee itakayoipa meno sera ya wazee katika utekelezaji wake, ikiwemo kuondoa changamoto zinazokabili kundi hilo.

Vile vile, limeitaka serikali kutoa mafao ya uzeeni kwa wazee wote waliotumika taifa kupitia serikalini au sekta binafsi.

Naye mwenyekiti wa baraza hilo, Hashim Juma Issa, ameishauri serikali kuunda chombo maalum kitakachoshughulikia matatizo ya wazee.

Amesema, “hii nchi ni kubwa sana na wazee wako wengi hivyo siyo rahisi kwa serikali kuwafikia wote, iwapo Chadema ikishika dola itaanzisha chombo cha kushughulikia changamoto za wazee.

Vile vile, inatakiwa kuwepo viti maalum kwa ajili ya wazee ili kundi hilo lipate wawakilishi wa kusemea changamoto zao bungeni.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!