Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga yaingiza Sh 404 mil
Michezo

Simba, Yanga yaingiza Sh 404 mil

Spread the love

Mchezo wa Ligi Tanzania bara namba 72, uliowakutanisha mabingwa watetezi Simba dhidi ya Yanga jana 30 septemba, 2018 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam umeingia Sh. 404,549,000 baada ya kuingiza watazamaji 50,168. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kwenye mgawanyo wa mapato hayo waliokuwa wenyeji wa mchezo huo klabu ya Simba wamepata kiasi cha Sh. 194,962,105, Bodi ya Ligi wamepata Sh. 29,244,315, gharama za mchezo ni Sh. 22,745,578, huku Baraza la Michezo lilipata Sh. 3,249,368  na Chama cha Mpira wa Miguu Dar es Salaam kiliambulia Sh. 9,748,105.

Lakini pia ghalama ya kodi ya ongezeko la thamani iliokwenda mamlaka ya mapatao Tanzania TRA ni Sh. 61,710,864.41 ambayo ni asilimia 18 ya fedha iliyopatikana huku wakala waliokuwa wakikatisha tiketi hizo za kieletroniki Selcom wao walipata Sh. 17,901,293.25.

Ikumbukwe mchezo huo uliisha kwa sare ya bila kufungana na hivyo kila timu kuambulia alama moja na kuendelea kubakia katika nafasi zao zilezile kwenye msimamo wa ligi kuu, Simba ikishika nafasi ya tano ikiwa na alama 10, huku Yanga ikisalia kwenye nafasi ya pili na kubakia na alama zao 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!