Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga yaingiza Sh 404 mil
Michezo

Simba, Yanga yaingiza Sh 404 mil

Spread the love

Mchezo wa Ligi Tanzania bara namba 72, uliowakutanisha mabingwa watetezi Simba dhidi ya Yanga jana 30 septemba, 2018 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam umeingia Sh. 404,549,000 baada ya kuingiza watazamaji 50,168. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kwenye mgawanyo wa mapato hayo waliokuwa wenyeji wa mchezo huo klabu ya Simba wamepata kiasi cha Sh. 194,962,105, Bodi ya Ligi wamepata Sh. 29,244,315, gharama za mchezo ni Sh. 22,745,578, huku Baraza la Michezo lilipata Sh. 3,249,368  na Chama cha Mpira wa Miguu Dar es Salaam kiliambulia Sh. 9,748,105.

Lakini pia ghalama ya kodi ya ongezeko la thamani iliokwenda mamlaka ya mapatao Tanzania TRA ni Sh. 61,710,864.41 ambayo ni asilimia 18 ya fedha iliyopatikana huku wakala waliokuwa wakikatisha tiketi hizo za kieletroniki Selcom wao walipata Sh. 17,901,293.25.

Ikumbukwe mchezo huo uliisha kwa sare ya bila kufungana na hivyo kila timu kuambulia alama moja na kuendelea kubakia katika nafasi zao zilezile kwenye msimamo wa ligi kuu, Simba ikishika nafasi ya tano ikiwa na alama 10, huku Yanga ikisalia kwenye nafasi ya pili na kubakia na alama zao 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!