Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yamlilia Thadei Ole Mushi
Habari za Siasa

CCM yamlilia Thadei Ole Mushi

Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimemlilia kada wake, Thadei Ole Mushi, aliyefariki dunia jana tarehe 4 Februari 2024, akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Salamu za rambirambi za CCM zimetolewa leo tarehe 5 Februari 2024 na idara yake ya itikadi, uenezi na mafunzo.

“CCM kimepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa taarifa ya msiba wa ndugu Thadei Ole Mushi, kilichotokea tarehe 4 Februari 2024 akiwa kwenye matibabu hospitalini jijini Dar es Salaam. Uongozi wa CCM chini ya mwenyekiti ndugu Dk. Samia Suluhu Hassan, unatoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki,” imesema taarifa hiyo.

Chama hicho kimesema kitamkumbuka marehemu Mushi kwa umahiri wake na uthubutu wa kukosoa bila woga.

“CCM kitamkumbuka kwa umahiri na uzalendo wa taifa lake, mchambuzi wa masuala ya kisiasa na alitumia maarifa na karama yake kutoa maoni na hisia zake katika nyanja nyingi za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Alikuwa kiongoni mwa vijana wachache wenye uthubutu, alisimamia alichokiamini hakuona soni kukosoa wala kukosolewa,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!