Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bulembo amshukia Polepole, ataka CCM amshughulikie
Habari za SiasaTangulizi

Bulembo amshukia Polepole, ataka CCM amshughulikie

Spread the love

MWENYEKITI Mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi, Abdallah Bulembo amemmshukia mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole akimtaka kumwacha, mwenyekiti wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan “amwache afanye majukumu yake kama Rais.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Bulembo aliyewahi kuwa mbunge wa kuteuliwa, amemwomba makamu mwenyekiti wa chama hicho-Bara, Philip Mangula kumchukulia hatua Polepole kwa matendo yake kama alivyowahi kuwahoji viongozi wengine wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Jumapili tarehe 12 Desemba 2021, amesema, “Lengo la Polepole ni kumkatisha tamaa Rais Samia. Hawezi ni mdogo sana. Rais Samia aachwe, namjua anaweza. Nimekaa naye namjua. Aachwe afanye kazi.”

Bulembo amesema, Polepole aliyewahi kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, “najiuliza Mzee Philip Mangula yupo wapi kwa hili linaloendelea kwa Polepole? Kama aliweza kuwahoji makatibu wakuu Wazee Makamba na Kinana, ameshindwa nini kwa huyu Polepole? Mimi naamini, Polepole analo jambo na ukitaka kufanya jambo, usiseme nishikeni nisipigane, wewe pigana tu.”

3 Comments

  • Hahahaaa kale kativii chake anacho fundishia uongozi usio wanafunzi bila vyeti, wahuni tumesha kilamba tumembakishia takataka zake tuu pamoja na kunguni wake, hivisasa tv ipo ktk familia nyengine tunamtazama Jot Online tv. next?…

  • Kwa kweli inasikitisha watu wasio na nguvu ya hoja kutumia tabia hii kwa visasi.
    Afrika haiwezi kuendelea kwa wivu wa aina hii.
    Naomba Hamisi Mgeja na Abdallah Bulembo mtoe tafsiri yenu ya “wahuni.” Msimwingize Mama Samia kwenye haya malumbano yenu. Mama hahusiki.
    Nyerere aliwahi kusema, “kukosoa na kukosoana, ni silaha ya mapinduzi.” Sisi tunataka kujifunza kwa hoja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!