Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bodi ya WRRB yaweka wazi mafanikio yake kwa mwaka 2021/22
Habari Mchanganyiko

Bodi ya WRRB yaweka wazi mafanikio yake kwa mwaka 2021/22

Mahindi
Spread the love

MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangya Bangu amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo kumeonesha kuwepo kwa mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja na wakulima kufurahia mfumo huo. Anaripori Danson Kaijage, Dodoma … (endekea).  

Ameyaeleza hayo leo tarehe 15 Februali, 2023 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari maelezo jijini hapa juu ya utekelezaji wa maendeleo katika mwaka wa fedha 2021/22.

Ameyataja mafanikio hayo ambayo yamepatikana toka kuanzishwa kwa mfumo huo wa Stakabadhi za Ghala ni pamoja na ongezeko la  bei za mazao, mapato ya mkulima na mapato ya Serikali kwa wastani wa asilimia 200% kutokana na urasimishaji.

Pia amesema mafanikio mengine ni ongezeko la uzalishaji wa mazao kwa wastani wa asilimia 20 kwa mwaka,  kichecheo cha ubora wa mazao yanayofikishwa sokoni, upatikanaji wa takwimu sahihi za mazao yanayopita kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Sambamba na mafanikio hayo amesema kuwa pia kumekuwepo na ongezeko la mapato ya uhakika kwa Serikali Kuu na Serikali Mitaa na kukuza huduma za fedha vijijini.

Sambamba na hilo amesema kuwa tangu mwaka 2007 hadi sasa kilo bilioni 2.3 za mazao ya nafaka zimepitishwa na bodi hiyo na kilo hizo zinatokama na mazao 11 yanayolimwa hapa nchini.

Hata hivyo Bangu amesema kuwa bodi inashirikiana na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima kwa lengo la kuwafanya wakulima kupata mazao bora na salama ambayo yataweza kuingia katika soko la ndani na nje ya nchi.

Aidha ameeleza kuwa bodi hiyo kwa sasa imekuwa ikishiriki kupata mazao ambayo hayapo katika bodi ili nayo yaweze kuingizwa katika ghala huku wakiangalia ni jinsi gani ya kuanzisha maghala ya mazao ya kuoza kama vile maparachichi na nyanya pamoja na mazao mengine.

Ukiachana na mazao hayo ameeleza kuwa kwa sasa bodi inafikilia na ipo katika mazungumzo na wizara ya mifugo ili kuweza kuanzisha maghala ya mifugo kama vile ngozi sambamba na mazao ya nyuki.

Hata hivyo amezitaja changamoto kadhaa kuwa ni pamoja na kukosekana kwa elimu juu ya mfumo ambao unatumiwa na bodi hiyo kwa kuwepo na maneno ya uzushi juu ya mfumo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!