Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bil 3.61 kutumika ujenzi barabara ya Lumecha – Londo
Habari Mchanganyiko

Bil 3.61 kutumika ujenzi barabara ya Lumecha – Londo

Spread the love

 

SERIKALI imetenga jumla ya Sh. 3.61 bilion kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Lumecha – Londo. Anaripoti Jemima Samwel DMC…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Godfley Msomgwe, Naibu Waziri wa Ujenzi leo Jumatatu tarehe 10 Mei 2021, katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, jijini Dodoma akijibu swali la Jacqline Msongozi, Mbunge wa Viti Maalumu.

 “Je, ni lini serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha Mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?” amehoji Msongozi.

Waziri Msongwe amesema, barabara hiyo ni sehemu ya barabara kuu ya Mikumi – Kidatu – Ifakara – Lupiro/Mahenge – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo – Lumecha yenye jumla ya kilometa 512, ambayo inaunganisha Mikoa ya Ruvuma na Morogoro.

“Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii, ulikamilika mwaka 2018 ikiwa ni lengo la serikali kujenga barabara yote kwa kiwango cha lami.

“Hadi sasa, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mikumi– Kidatu (km 35.2) na ujenzi wa Daraja la Magufuli (m 384) pamoja na barabara unganishi (km 9.142), umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya Kidatu – Ifakara (km66.9) unaendelea na umefikia asilimia 22.6,” Waziri Msongwe amesema.

Amesema, kwa upande wa barabara hiyo kuanzia Lupiro/Mahenge – Malinyi– Kilosa kwa Mpepo – Londo – Lumecha, serikali inaendelea kutafuta fedha za kuanzaujenzi kwa kiwango cha lami ikiwemo sehemu ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo.

“Wakati juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami zikiendelea, serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Ruvuma na Morogoro itaendelea kuifanyia matengenezo barabara hii kutoka Ifakara – Lupiro/Mahenge – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo – Lumechakila mwaka ili iweze kupitika majira yote ya mwaka.

“Katika mwaka wa fedha 2020/21, barabara hii imetengewa jumla ya Sh.361.51 Milioni kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. Kati ya fedha hizo, Sh. 985.58 milioni ni kwa ajiliya sehemu ya barabara ya Lumecha – Londo ambayo iko mkoa wa Ruvuma,” amesema Msongwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!