Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Biashara United kupaa leo, kuwavaa wadjibout
Michezo

Biashara United kupaa leo, kuwavaa wadjibout

Spread the love

 

KLABU ya soka ya Biashara United ya mkoani Mara inatarajia kuondoka leo 9 septemba 2021majira ya saa 10:00 jioni chini kuelekea nchini Djibout kwa ajiri ya mchezo wake wa kwanza wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya klabu ya Dhikhil Fc. Anaripoti Damas Ndelema TUDARCo(endelea)

Mchezo huo wa hatua ya awali utapigwa kesho, majira ya saa 10 jioni, kwenye Uwanja wa Stade du ville.

Hapo awali Biashara United ilitakiwa kuondoka nchini siku ya jana kwenda nchini Djibout lakini ilishindikana kutokana na baadhi ya wachezaji kuchelewa kutoka kwa hati zao za kusafiria  jambo lililofanya safari hiyo kukwama  hivyo klabu hiyo itaondoka nchini siku ya leo.

Kwa mujibu wa meneja na mratibu wa klabu ya Biashara United , Frank Wambare alisema kuwa, sasa wataondoka kesho (leo) Septemba 9, 2021 majira ya saa 10 jioni kupitia Uwanaj wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.

‘’Tunatarajia kuondoka nchini  siku ya alhamisi 9 septemba kuelekea nchini Djibout majira ya saa10:00 jioni ili kuwahi mchezo wetu utakao chezwa siku ya ijumaa tarehe 10 septemba ‘’. Alisema Meneja

Klabu hiyo itaondoka na jumla ya wachezaji 30 pamoja na benchila ufundi na hakuna mchezaji yeyote alie ripotiwa kuwa majeruhi.

Biashara itakabiliana na klabu ya Dhikhil Fc katika hatua ya  awali ya kombe la shirikisho kwa kuanzia ugenini kisha itarejea kucheza itaikaribisha nyumbani timu hiyo baada ya wiki mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!