KLABU ya soka ya Biashara United ya mkoani Mara inatarajia kuondoka leo 9 septemba 2021majira ya saa 10:00 jioni chini kuelekea nchini Djibout kwa ajiri ya mchezo wake wa kwanza wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya klabu ya Dhikhil Fc. Anaripoti Damas Ndelema TUDARCo(endelea)
Mchezo huo wa hatua ya awali utapigwa kesho, majira ya saa 10 jioni, kwenye Uwanja wa Stade du ville.
Hapo awali Biashara United ilitakiwa kuondoka nchini siku ya jana kwenda nchini Djibout lakini ilishindikana kutokana na baadhi ya wachezaji kuchelewa kutoka kwa hati zao za kusafiria jambo lililofanya safari hiyo kukwama hivyo klabu hiyo itaondoka nchini siku ya leo.
Kwa mujibu wa meneja na mratibu wa klabu ya Biashara United , Frank Wambare alisema kuwa, sasa wataondoka kesho (leo) Septemba 9, 2021 majira ya saa 10 jioni kupitia Uwanaj wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.
‘’Tunatarajia kuondoka nchini siku ya alhamisi 9 septemba kuelekea nchini Djibout majira ya saa10:00 jioni ili kuwahi mchezo wetu utakao chezwa siku ya ijumaa tarehe 10 septemba ‘’. Alisema Meneja
Klabu hiyo itaondoka na jumla ya wachezaji 30 pamoja na benchila ufundi na hakuna mchezaji yeyote alie ripotiwa kuwa majeruhi.
Biashara itakabiliana na klabu ya Dhikhil Fc katika hatua ya awali ya kombe la shirikisho kwa kuanzia ugenini kisha itarejea kucheza itaikaribisha nyumbani timu hiyo baada ya wiki mbili.
Leave a comment