Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Hashimu Mgandilwa akizungumza na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya wateja wake jijini Tanga.
IKIWA ni muendelezo wa utaratibu wake wa kuandaa futari kwa ajili ya wateja na wadau wake katika mikoa mbalimbali nchini kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Benki ya EximTanzania mwishoni mwa wiki iliandaa futari maalum kwa ajili ya wateja wake mkoani Tanga. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hafla ya futari hiyo ilifanyika Hotel ya Tanga Beach Resort jijiji Tanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo wateja, wafanyakazi wa benki hiyo.
Pia viongozi mbalimbali wa serikali walihudhuria wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Hashimu Mgandilwa pamoja na Sheikh Mkuu wa Mkoa huo, Juma Luwuchu.
Leave a comment