Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bashe: Naweza kuhama CCM kama Lowassa
Habari za SiasaTangulizi

Bashe: Naweza kuhama CCM kama Lowassa

Spread the love

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Bashe anaweza kuondoka kwenye chama hicho pale kitakapoboronga. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Amesema kuwa, anaweza kufanya hivyo kama alivyofanya Edward Lowassa, Maalim Seif Sharif Hamad na hata Augustino Mrema. 

Bashe ambaye ni Mbunge wa Nzega Mjini amesema hayo kwenye mkutano wa kampeni katika Jimbo la Ukonga wakati wa kumnadi mgombea wa chama hicho, Mwita Waitara leo Septemba 12,  2018.

Amesema kuwa, kuhama chama sio dhambi na kwamba alichokifanya Waitara ni haki yake kama walivyofanya wengine wakitoka CCM.

Mbunge huyo kijana anapishana mtazamo na wale wanaosema kuwa, Waitara alinunuliwana na CCM na kwamba, hoja hiyo ni dhaifu.

“Waitara namfahamu toka alipojuwa Umoja wa Vijana wa CCM-UVCCM” amesema Bashe na kuongeza:

“Aliondoka Mzee Augustine Mrema mwaka 1995, Maalim Seif naye akaondola hadi mzee wangu Lowassa alifanya hivyo, hatujawahi kutuhumu kama mtu amenunuliwa.

“Yoyote anapoamua kuwatumikia wananchi anapanda basi, vyama vya siasa ni sawa na basi, ukiona basi hilo dereva, kondakta hamuelewani unaweza kushuka kwenye basi hilo.”

Wakazi wa Jimbo la Ukonga wanatarajiwa kumchagua mbunge wao baada ya Waitara kujivua ubunge na kujiunga CCM ambayo imempitisha kugombea kwenye uchaguzi huo mdogo utaofanyika Jumapili ya Septemba 16 mwaka huu.

Jimbo lingine linalotarajiwa kufanyika uchaguzi siku hiyo ni Monduli pamoja na kata 22 nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!