Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bashe: Hakuna Mtanzania atakayekosa chakula
Habari Mchanganyiko

Bashe: Hakuna Mtanzania atakayekosa chakula

Mahindi
Spread the love

 

SERIKALI imesema kuwa pamoja na kuwepo kwa mabadiko ya tabia ya nchi yaliyosababisha kukosekana kwa mvua za uhakika, nchi ina akiba ya chakula cha kutosha. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 22 Januari, 2022 na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe jijini Dodoma alipokutana na wasambazaji wa mbolea kwa lengo la kujadili bei ambayo inampa unafuu mkulima.

Amesema kuwa hakuna Mtanzania atakayekufa na njaa kwa kuwa serikali ina akiba ya chakula cha kutosha tani 200,000 za mahindi.

Bashe amesema hawatawapa wafanyabiashara wauze tani hizo za mahindi.

Amesema serikali kupitia Halmashauri husika watafungua vituo na mahindi ambayo yatauzwa kwa bei nafuu ili wananchi wakidhi na kupata mahitaji yao.

“Wananchi ambao wanaakiba ya chakula waendelee kuhifadhi kwa sababu tunaweza tusipate chakula kama mwaka jana.

“Tathimini ya awali inaonesha uzalishaji wetu pamoja na upungufu wa mvua tulikuwa na wastani wa asilimia 125 hadi 127 lakini kipindi hiki kinaweza kushuka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa,” amesema Bashe.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Waziri Bashe ameongeza kama serikali wanafahamu bei ya mbolea imepanda na msimu wa mvua za vuli zimeanza na kuna baadhi ya wakulima walitarajia kupanda licha ya upungufu wa mvua.

“Baadhi ya maeneo nchini mvua zimeanza kunyesha za masika Taarifa za Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania (TMA), zinatarajiwa mwezi huu mwishoni kutakuwa na mvua hadi Februari,” ameeleza.

Amesema maeneo ambayo ni ya mvua chini ya wastani serikali imeanza kuchukua hatua ya kuhakikisha njia mbadala za zao ambalo linaweza kuwasaidia wakulima kupata kipato.

Bashe amefafanua kuwa tayari Serikali imegawa mbegu za alizeti katika maeneo yenye mvua za wastani zaidi ya tani 1600.

Ameongeza kuwa maeneo mingine ambayo yana mvua chini ya wastani waendelee kuwasiliana na wizara kwa ajali ya kuendelea kuwapatia mbegu ambazo watazigawa kwa wakulima wapate zao ambalo litawapatia kipato na yenye kustamili ukame.

Waziri huyo amesema wametoa miongozo ya aina ya mazao ambayo yanaweza kuvumilia ukama yakiwamo mtama na mihogo katika kila mikoa.

Bashe amesema uzalishaji wa chakula umekabiliwa na bei ya mbolea na serikali inafahamu miaka ya 2015 hadi 2017 ilikuwa ikitoa ruzuku za pembejeo .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!