Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Babu Seya atinga Ikulu kumshukuru Rais Magufuli
Habari za Siasa

Babu Seya atinga Ikulu kumshukuru Rais Magufuli

Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza wakiwasili Ikulu
Spread the love

Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha” Francis Nguza na Michael Nguza leo wamefika Ikulu kumshukuru Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa msamaha aliotoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia gerezani, anaandika Hamis Mguta.

Rais Magufuli alitoa msamaha huo Disemba 9 mwaka jana, akiwa Dodoma katika sherehe za miaka 56 ya Uhuru.

Mwaka 2003, Babu Seya na wanaye watatu walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Mashujaa ambapo mwaka 2004, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar iliwahukumu wote wanne kifungo cha maisha jela.

Baada ya hukumu hiyo, walikata rufaa lakini mwaka 2005, Mahakama Kuu iliridhia hukumu hiyo ya kifungo cha maisha jela kwa wote wanne kabla ya Mahakama ya Rufaa kuwaachia huru watoto wawili wa Nguza – Mbangu “Nguza Mashine” na Francis  Nguza “Chichi” mnamo Februari 2010.

Nguza amesema “Muheshimiwa rais alinisamehe kule, nimekuja kutoa shukrani zangu za dhati kutoka ndani ya moyo wangu na kumuomba aniruhusu sasa kuanza kufanya kazi.

“Kuanzia sasa nipo huru kufanya kazi, mashabiki wanipe muda kidogo nitawatangazia lini nitanza kuingia jukwaani.”

 

1 Comment

  • Rais amewasamehe kama alivyodai kwa mujibu wa sheria. Asimsingizie Mungu kuwa ndiye aliyesamehe
    Lakini kina Babu Seya nao wameomba msamaha kwa watoto waliowalawiti? Utamsamehe vipi mtu ambaye hajaomba msamaha?
    Nashauri Rais sasa akutane na watoto waliolawitiwa na wazazi wao. Hawa ndio waliodhulumiwa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!