MAMLAKA ya mawasiliono nchini TCRA imetoa hukumu kwa televisheni nne kwa tuhuma za uchochezi na kukiuka kanunuzi za utangazaji, Anaripoti Faki Sosi….(endelea)
Mamlaka hiyo kupitia timu yake ya kamati ya maudhui imevipa adhabu ya kulipa faini kituo cha televisheni Star tv, Azam tv Channel ten pamoja na East Africa Tv.
Akisoma hukumu hiyo hiyo Makamo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Joseph Mapunda amesema kuwa vituo hivyo vimefanya uchochozi kwa kutangaza habari ya kituo cha sheria na haki za binaadamu kilipokuwa klikitoa tathimini ya uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 uliofanyika Novemba 30 mwaka 2017 sehemu mbalimbali nchini.
Taarifa ya Kituo cha sheria na haki za binadamu ileelza kuwa waangalizi wa kituo hicho walifika sehemu mbalimbali zilizofanyika uchaguzi huo na kubaini uvunjwaji wa haki za binadamu, utekwaji na upigwaji wa watu umejitokeza kwenye uchaguzi huo na kwamba vitendo hivyo vimetekelezwa na vyomvo vya dola pamoja na wafuasi wa vyama mbalimbali vya siasa.
Mapunda ameendelea kusema kuwa vyombo hivyo vilitangaza taarifa hizo bila kuthibitisha ukweli wa taarifa hiyo kwa kuzungumza na wahusika wa wa mamlaka zilizotuhumiwa kama vile Tume ya uchaguzi NEC au jeshi la Polisi.
Amesema kuwa vyombo hivyo vimepewa adhabu hiyo kutokana kukiuka kanuni za utangazaji , kutangaza habari za uchochezi zingeweza kuhatarisha usalama wa taifa, kutangaza habari ambazo hazikutibitishwa ukweli wake pamoja na kushindwa kufanya mizania
Hivyo vituo hivyo vimepewa adhabu ya kulipa faini, vituo hivyo ni pamoja na azamu kulipa shilingi 7.5 milioni, Star tv Shilingi 7.5 milioni na East Afrika tv Shilingi Mil 15milioni pamoja na channel ten 15 milioni.
Mapunda amesema kuwa faini hiyo italipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo tarehe 2 januari licha kuwepo wazi kwa rufaa kwa wamiliki wa vyombo hivyo kwa muda wa siku 30 pamoja na kuwekwa chini ya uangalizi kwa muda wa miezi sita kuanzia sasa.
hata wakikata rufaa wasikiliza rufaa ndo hao hao hakuna haki itakayo tendeka,