Rais wa chama cha Wachungaji na Maaskofu nchini, Tanzania Pastors Association (TPA) Askofu Dr Mussa Mlawi ambaye pia ni Askofu mkuu wa Kanisa la Spiritual Pentecoste Church of Tanzania. (SPCT). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kwa ujasiri wake wa kuamua kuwa msingi imara wa Haki, Demokrasia na Maendeleo kwa Watanzania bila kujali Itikadi zao..
Askofu Mlawi amesema; Tanzania ya Rais Samia imekuwa sehemu salama kwani hakuna hofu kama awamu zilizopita na sasa Wananchi wanamhitaji zaidi Rais Samia kwani kwa muda mchache amefanya mambo makubwa licha ya kubezwa na baadhi ya watu waliyoamini asingeweza kuwa kiongozi imara, mwenye ushawishi na mvuto kwa wananchi, Rais Samia amekuwa bora kuliko wengi walivyodhani.
Rais Samia ni dhahabu iliyokuwa ndani ya gunia la mkaa, wengi haliipuuza lakini sasa imejidhihilisha kuwa ni dhahabu nasi mkaa. Wafanyakazi wameongezwa mshahara kwa kiwango kikubwa, ujenzi wa miundombinu pamoja na kujenga Mahusiano mazuri baina yetu na mataifa mengine kunatufanya hata sisi wengine tuseme, sasa Tanzania inaye Rais. Amesema Askofu Dr Mussa Mlawi.
Leave a comment