Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Askofu awatwisha mzigo wa Corona waandishi wa habari
AfyaHabari Mchanganyiko

Askofu awatwisha mzigo wa Corona waandishi wa habari

Spread the love

ASKOFU Evance Chande wa Kanisa la EAGT Dodoma, ameviomba vyombo vya habari na waandishi wa habari kutoa elimu ya maambukizi ya corona kwa wananchi waishio vijijini. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Askofu Chande ametoa kauli hiyo wakati wa Ibada ya kumbukizi ya kufufuka kwa Yesu Kristo iliyofanyika kanisani hapo lililipo Ipagala Jijini hapa.

Alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo kwa sasa ni kutokuwepo kwa elimu ya kutosha hasa watu waishio vijijijini.

Akihubiri kanisani hapo alisema iwapo waandishi nao watatumia nafasi yao kwenda vijijini kwa ajili ya kusaidia jamii juu ya kujikinga na maabukizi hayo watakuwa wameisaidia serikali kwa hatua kubwa.

“Hapa mtaona kuwa baada ya Serikali kutangaza kuwepo kwa ugonjwa huo waandishi wa habari na vyombo vya habari vilijitahidi na vinaendelea kujitahidi kutangaza jambo ambalo limesababisha kila mmoja kujua kinachoendelea.

“Vyombo vya habari na waandishi wa habari kwa kutumia weledi wao wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa jamii kwa kutoa elimu hata maeneo ambayo hayafikiki,”alisema Askofu Chande.

Katika hatua nyingine amewakemea baadhi ya watu ambao wanafanya mzaa na janga hilo la Corona na kuwataka kuacha mara moja na badala yake wazingatie maelekezo ya Serikali.

Alisema Ugonjwa wa Corona siyo wa mchezo na ni janga la Kidunia hivyo ni muhimu kuhakikisha jamii inazingatia maelekezo ya wataalamu wa Afya.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya kumbukizi ya kufufuka Yesu Kristo alisema siku hiyo isitumiwe kufanya anasa badala yake siku hiyo iwe siku ya kumtafakari Mungu.

Katika hatua nyingine amewaagiza watanzania kwa ujumla wake wakakikishe kwenye majumba yao wanaweka vitakatisha mikono ili wanapotembelewa na wageni wawezi kunawa Kama yalivyo maelekezo ya Serikali.

Naye Askofu wa Kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania (PHAMT), Jimbo la Kanda ya Kati, Julias Bundala aliiomba serikali kuongeza ulinzi mipakani ili kukabiliana na watu ambao wanaingia nchini na Virusi vya Ugonjwa wa Corona.

Mbali na hilo alisema kuwa serikali iangalie namna bora ya kuwapatia huduma waliowekwa karantini ili wanapokuwa katika ungalizi wa siku 14 wasitoke na badala yake huduma ziwakute hapo hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!