Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Janga la Corona:Tanzania yazuia safari za ndege kimataifa
AfyaHabari Mchanganyiko

Janga la Corona:Tanzania yazuia safari za ndege kimataifa

Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TCAA), imefuta safari za ndege za abiria za kimataifa, huku ikiweziwekea masharti ndege za mizigo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Zuio hilo limetolewa na TCAA jana tarehe 11 Aprili 2020, huku ikieleza sababu zake kuwa ni kudhibiti kasi ya ueneneaji Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19).

Kwa mujibu wa taarifa ya TCAA, zuio hilo litadumu hadi mamlaka hiyo itakapotoa taarifa zaidi.

“Kutokana na janga la COVID-19, vikwazo vifuatavyo vimechukuliwa kuanzia Aprili 11 2020 hadi taarifa zaidi itakapotolewa. Ratiba zote za safari za kimataifa zimesitishwa,” inaeleza taarifa ya TCAA.

TCAA imeeleza kuwa, ndege za mizigo zitaruhusiwa kufanya safari, lakini zitapaswa kuwa na watu wachache ambao watawekwa karantini na serikali,  kwa gharama zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

error: Content is protected !!