Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Biashara ASAS Dairies yajitosa kuokoa afya za watoto wadumavu Z’Bar
Biashara

ASAS Dairies yajitosa kuokoa afya za watoto wadumavu Z’Bar

Spread the love

KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapindizi Zanzibar za kumaliza tatizo la udumavu kwa watoto  kampuni ya Asas Dairies  imezindua programu ya unywaji wa maziwa kwa wanafunzi wa shule visiwani hapa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar …(endelea).

Uzinduzi wa Programu hiyo unefanyika jana tarehe 26 Agosti 2023 na Ahmed Salim Asas Mkurugenzi wa kampuni hiyo mbele ya Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi aliyeonesha kufuhishwa na mpango huo wenye lengo  kuimarisha afya za wananchi wote.

 

Ahmed Asas alimueleza Rais Mwinyi kuwa kwa kuanzia wamepanga kugawa zaidi ya lita 5,000 kwenye Shule zaidi ya 25 visiwani hapa.

Alisema hatua hiyo imekuja kufuatia ripoti ya mwaka jana iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuonyesha asilimia 1.8 ya watoto Zanzibar wana tatizo la udumavu jambo lililowapalekea kushirikiana na Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu kufanya jitihada za kupunguza na ikiwezekana kumaliza tatizo hilo.

Pamoja na hayo alisema lengo lingine la program hiyo ni kuimarisha lishe na Afya za Wanafunzi na Wananchi kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa mwaka mtu Mmoja anatakiwa kunywa Maziwa yasiyopungua lita 200 lakini kwa sasa takwimu zinaonyesha hali ya unywaji maziwa nchini sio ya kuridhisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza sloti ya Zombie Apocalypse na ushinde kirahisi

Spread the love Wengi wetu hupenda filamu za Mazombie huwa zinatishakidogo lakini...

Biashara

Ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu katika utekelezaji wa sera za afya na usalama kazini

Spread the love  KILA ifikapo Aprili 28 ya kila mwaka, dunia huadhimisha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Biashara

Wazir Jr kinara wa ufungaji KMC FC ajiunga Meridianbet

Spread the love    MUITE Wazir Jr ‘The King of CCM Kirumba’,...

error: Content is protected !!