Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU
Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the love

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi mambo yaliyoibuliwa katika Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  na taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 28 Machi 2024, Ikulu jijini Dodoma baada ya kupokea ripoti hizo alizokabidhiwa na CAG Charles Kichere na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum Hamduni.

“Ripoti hizi zinazosomwa kila mwaka zinachangia maboresho au kuimarisha utendaji ndani ya serikali na mashirika ya umma, kuna dosari zilizotolewa hapa tutaenda kuzifanyia kazi kisawasawa turekebishe na mwakani pengine hizi hazitajirudia tutakuwa tumesogea,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amesema ripoti hizo zinaonesha kwamba kuna maboresho yaliyofanyika katika masuala ya usimamizi wa fedha za umma kwani ripoti ya CAG imeonesha hati safi zimeongezeka hadi kufikia asilimia 99, wakati hati chafu ikiwa ni moja.

Ripoti ya CAG imeibua madudu katika baadhi ya mashirika ya umma na mamlaka za serikali za mitaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!