Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ripoti ya CAG yatinga bungeni
Habari za Siasa

Ripoti ya CAG yatinga bungeni

Spread the love

RIPOTI kuu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2023, imewasilishwa bungeni jijini Dodoma, kwa ajili ya kujadiliwa na wabunge. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ripoti hiyo imewasilishwa leo tarehe 15 Aprili 2024, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande, ikiwa ni wiki mbili baada ya CAG Charles Kichere, kuikabidhi kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, tarehe 28 Machi mwaka huu.

Akiwasilisha hati ya ripoti hiyo mezani, Chande amesema imebeba ripoti 21 za ukaguzi, ikiwemo ripoti ya CAG kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za Serikali kuu, ripoti kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za mamlaka za serikali za mitaa, ripoti ya ukaguzi wa taarifa za fedha za miradi ya kimkakati na ripoti ya ukaguzi wa mashirika ya umma.

Ripoti nyingine ni ya ukaguzi wa ufanisi na ripoti ya ukaguzi wa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!