Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makala: Puuzeni wanasiasa wanaojigamba wanaweza kubadili maamuzi ya mahakama
Habari za Siasa

Makala: Puuzeni wanasiasa wanaojigamba wanaweza kubadili maamuzi ya mahakama

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Amos Makala
Spread the love

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makala, amewataka wananchi wenye madai ya haki ambayo hayajafikishwa mahakamani kuwasilisha migogoro yao kwa viongozi wa chama hicho ili wapate msaada. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa CCM mkoani Katavi, leo Jumamosi, Makala amewataka wananchi kupuuza wanasiasa wanaowaeleza kwamba wana uwezo wa kubadili maamuzi ya mahakama.

“Changamoto za Katavi nazijua, unaambiwa hili liko mahakamani, asije mwanasiasa akakudanyanga kwamba anaouwezo wa kubadili maamuzi ya mahakama akakupa haki, wote tunaamini kwamba chombo ambacho kikatiba cha kutoa haki ni mahakama,” amesema Makala na kuongeza:

“Sisi tuko tayari kusikiliza kero zozote ambazo bado hazijaingia kwenye mhimili wa mahakama, tutawasaidia wananchi wanyonge katika mambo ambayo bado hayajaingia katika mahakama ili apate haki hiyo na wale ambao wako mahakamani ushauri mkubwa kama ulikosa haki mahakama ya chini ukate rufaa mahakama ya juu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!