Wednesday , 22 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa
Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the love

Spika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huku kukiwa na uchunguzi wa tuhuma za rushwa wakati akiwa waziri wa ulinzi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hayo yanajiri baada ya wiki iliyopita nyumba ya Spika huyo kuvamiwa na maofisa upelelezi, ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa tuhuma hizo za rushwa.

Akitangaza kujiuzulu jana Jumatano, Mapisa-Nqakula alisema; “Kujiuzulu kwangu sio dalili au kukubali hatia kuhusiana na tuhuma zinazotolewa dhidi yangu.”

Kujiuzulu huko, ambako kunaanza kutekelezwa mara moja, pia kunaambatana naye kuacha kazi kama mbunge.

Mapisa-Nqakula alikuwa waziri wa ulinzi nchini humo kuanzia mwaka 2012 hadi 2021.

Shirika la utangazaji la serikali ya Afrika Kusini (SABC) liliripoti kwamba anatuhumiwa kupokea mamilioni ya pesa taslimu kama hongo kutoka kwa wakandarasi wa zamani wa kijeshi.

Mapisa-Nqakula alichukua likizo maalum baada ya uvamizi huo na juzi Jumanne, ombi lake kwa mahakama kuzuia mamlaka kumkamata, lilitupiliwa mbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

Habari za SiasaKimataifa

Balozi Kasike ateta na mjumbe wa FRELIMO

Spread the loveBalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji, Phaustine...

error: Content is protected !!