Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtuhumiwa wa utapeli, kudhulumu viwanja aburuzwa mahakamani
Habari MchanganyikoTangulizi

Mtuhumiwa wa utapeli, kudhulumu viwanja aburuzwa mahakamani

Spread the love

Mtuhumiwa wa kutapeli na kudhulumu viwanja vya watu na kujimilikisha kinyume na utaratibu jijini Dar es salaam ajulikanae kama Paul Mushi leo Ijumaa ametolewa kituo cha Polisi Oysterbay na kupelekwa mahakama ya mwanzo Kinondoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya mtuhumiwa huyo kukamatwa hapo awali kwa tuhuma za kunyang’anya viwanja vya watu kadhaa na sasa amepekwa mahakamani ili hatua za kisheria ziendelee.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa

Aidha, mapema jana Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa alitangaza kuanza kwa operesheni maalumu ya kudhibiti matapeli wa ardhi katika jiji la Dar es salaam.

Operesheni hii imekuja siku chache tangu kufanyika kwa Kliniki ya Ardhi ya Jijini Dar es salaam iliyoanza mapema mwezi Novemba 2023 na kuhitimishwa tarehe 3 Machi 2024 kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi iliyokuwa inasumbua jiji la Dar es salaam kwa muda mrefu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!