Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Chalamila: Samia ameruhusu maandamano Chadema
Habari za SiasaTangulizi

RC Chalamila: Samia ameruhusu maandamano Chadema

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila
Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kufanya maandamano yao kwa amani bila kuharibu miundombinu ya Jiji hilo kwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameruhusu maandamano hayo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Chalamila ametoa wito huo leo tarehe 24 Januari 2024, alipowasili maeneo ya Stendi ya Magufuli, Mbezi Mwisho, ambako wafuasi na viongozi wa Chadema wakiongozwa na makamu wao mwenyekiti bara, Tundu Lissu wanatarajia kuandamana kuelekea ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN).

“Mnatakiwa kufikisha ujumbe pale mlipokusudia, serikali tuko na nyie na tunawatakia kila la heri, ninyi na mimi ni wana Dar es Salaam penye mzunguko mkubwa wa pesa, hospitali kubwa na uwekezaji mkubwa, maandamano yetu yanapaswa kulinda uwekezaji wote huo, Rais @samia_suluhu_hassan  na viongozi wote wamesema wacha watu waandamane,” amesema Chalamila.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, Benson Kigaila, alimtaka kiongozi huyo wa Dar es Salaam, kutovuruga maandamano Yao.

Chadema wanatarajia kuanza maandamano Yao katika maeneo mawili, Mbezi Mwisho atakakoongoza Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na Buguruni Sheli atakakoongoza Mwenyekiti Freeman Mbowe.

Chama hicho kimeitisha maandamano hayo ili kuishinikiza serikali kuiondoa bungeni jijini Dodoma miswada ya marekebisho ya Sheria za uchaguzi, wakidai kuwa ni mibovu.

Pia, wanadai miswada huyo haijabeba mapendekezo yaliyotolewa na wadau kuhusu maboresho ya mifumo ya uchaguzi.

1 Comment

  • Duh! Hongera Mama Dk. Samia Suluhu Hassan. Umeonyesha ukomavu wa kisiasa kutoogopa maandamano kama wakoloni na viongozi waliokutangulia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!