Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waanza kuwasili vituo vya maandamano, Mbowe kuongoza Buguruni
Habari za SiasaTangulizi

Chadema waanza kuwasili vituo vya maandamano, Mbowe kuongoza Buguruni

Spread the love

BAADHI ya viongozi na wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameanza kuwasili maeneo ya Buguruni Sheli jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kushiriki maandamano yanayotarajiwa kuongozwa na Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Licha ya mvua kunyesha hapa na pale, leo tarehe 24 Januari 2024, wanachama hao wa Chadema walianza kuwasili katika eneo hilo kuanzia majira ya saa 12 asubuhi, ambapo maandamano yanatarajiwa kuanza rasmi saa 3.00 asubuhi.

Hadi sasa viongozi wa Chadema waliofika katika eneo hilo ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Chadema, Mzee Hashim Juma na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Joseph Mbilinyi (Sugu) na Naibu Katibu Mkuu Bara, Benson Kigaila

Akizungumza na MwanaHALISI Online,  Mzee Hashim amesema kwa sasa wanamsubiri Mbowe afike ndio waanze maandamano hayo.

Aidha, amesema magari yametumwa kwenda kuwafuata wanachama katika majimbo yao ili kuwaleta eneo la tukio.

“Kiongozi wa msafara atakuwa Mbowe na msafara wetu unaanza saa tatu kamili asubuhi,mwitikio wa watu ni mkubwa na wengine wako njiani wanakuja hapa ili tukutane kwa ajili ya kuanza msafara,” amesema Mzee Hashim.

Mzee Hashim amesema kabla maandamano hayo hayajaanza wameshaona matokeo chanya, ikiwemo wanajeshi waliotajwa kufanya usafi siku ya leo kutoonekana barabarani kitendo alichoita kwamba Serikali imeheshimu uamuzi wao wa kufanya maandamano.

Pia, amesema mafanikoo mengine ni Umoja wa Mataifa (UN), kuwa tayari kuwapokea.

Kwa upande wake Sugu amesema anatarajia watanzania watatoka majumbani kwenda kujumuika nao.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema Arusha,  Emma Kimambo, amesema maandamano hayo yatasaidia kufikisha malalamiko ya wananchi Kwa Serikali hasa ugumu wa maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!