Sunday , 12 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar wadaka watuhumiwa usambazaji picha za ngono
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar wadaka watuhumiwa usambazaji picha za ngono

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linawashikilia watu wawili wanaotuhumiwa kuwapa dawa za kulevya wanawake bila kujijua kisha kuwapiga picha za utupu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 19 Disemba 2023 na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, akizungumzia operesheni maalum ya kuwakamata wahalifu iliyoanza kufanyika Septemba mwaka huu.

Kamanda Muliro amesema watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na vitu mbalimbali walivyoiba ikiwemo kompyuta mpakato (laptop) 10, simu za mkononi 305, televisheni 36, kamera 4 na makava ya simu 160.

“Katika maeneo mbalimbali jijini tumewanasa watuhumiwa wakiwemo watu wawili ambao majina yamehifadhiwa kwa sababu za uchuguzi. Huwatongoza wanawake, wanawawekea dawa za kuwalewesha, kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji wa kingono na kuwapiga picha, kuwatishia kuwaua wakitoa siri za udhalilishaji huo na baadae kuwaibia simu, laptop na fedha,” amesema Kamanda Muliro.

Katika tukio lingine, Kamanda Muliro amesema watu watatu, Msabaha Michael, Juma Athumani na Joseph Januari, wanashikiliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano kufuatia tuhuma za wizi wa vifaa vya boti inayomilikiwa na raia wa Afrika Kusini, Van Baurenm.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!