Wednesday , 22 May 2024
Home Kitengo Biashara Bei ya Dizeli, Petroli yashuka
BiasharaTangulizi

Bei ya Dizeli, Petroli yashuka

Spread the love

BEI ya mafuta kwa mwezi Disemba, imeshuka kutokana na kupungua kwa bei za mafuta ghafi kwenye soko la dunia, pamoja na  gharama za kuagiza nishati hiyo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dk.James Mwainyekule, bei ya mafuta ya petrol imepungua kwa asilimia 0.89, ikiwa ni wastani wa Sh. 116, huku upande wa dizeli yakishuka kwa asilimia 9.11, sawa na wastani wa Sh. 148, kwa kila lita.

Taarifa hiyo imeonesha viwango elekezi vya bei ya mafuta, ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam, bei impungua kutoka Sh. 3,274 iliyokuwa Novemba hadi kufikia Sh. 3,158, inayoanza kutumika leo tarehe 6 Disemba mwaka huu.

Kwa upande wa bei ya mafuta ya taa, imebaki kama ilivyo.

“Mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi Desemba 2023 yanatokana na kupungua kwa bei za mafuta ghafi katika soko la dunia kwa wastani wa asilimia 8.72% na gharama za uagizaji wa mafuta kwa wastani wa asilimia 27 kwa petroli na asilimia 23 kwa dizeli,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Hukumu mahakama kuu yabatilishwa kesi State Oil, Equity Bank Tz

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imebatilisha hukumu iliyotolewa...

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

BiasharaElimu

Benki ya Exim yazindua huduma ya ‘Exim Smart Shule’

Spread the love  KATIKA juhudi za kuboresha teknolojia za kidijitali katika sekta...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

error: Content is protected !!