Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bashungwa aahidi Tanzania Bara, Zanzibar kudumisha ushirikiano sekta ya ujenzi
Habari Mchanganyiko

Bashungwa aahidi Tanzania Bara, Zanzibar kudumisha ushirikiano sekta ya ujenzi

Spread the love

WAZIRI wa  Ujenzi, Innocent Bashungwa ameahidi kuendelea kudumisha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya ujenzi  ili uboreshaji wa miundombinu ya ujenzi upatikane katika maeneo yote ya bara na visiwani. Anaripoti Danson Kaijage, Mwanza (endelea).

Bashungwa ametoa kauli hiyo jana jijini Mwanza katika mkutano wa sita wa sekta hiyo uliobeba kauli mbiu ya “Ushirikiano imara kwa miundombinu na muungano imara”.

Pia ameahidi kusimamia kwa karibu mapendekezo na maazimio yote waliyokubaliana katika mikutano inayofanyika kwa faida ya pande zote mbili za muungano.

Aidha, Bashungwa amempongeza Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi kwa kutimiza miaka mitatu tangu aingie madarakani.

Amesema katika kipindi hicho kumekuwa na mageuzi makubwa kwenye sekta ya ujenzi ambayo ni kichocheo kikubwa katika ukuaji wa sekta ya utalii, elimu na afya na hivyo kukuza uchumi wa Taifa kiujumla.

Naye Mwenyekiti mwenza kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi (SMZ), Dk. Khalid Mohamed amesema kwa kuzingatia kazi za Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi, sekta ya ujenzi imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema  miundombinu katika pande hizo mbili imeshamiri na hivyo kuchochea ukuaji wa utalii na hivyo kukuza uchumi wa taifa.

“Kwa kipindi cha miaka mitatu cha uongozi wa Rais Dk. Mwinyi tumepata mafanikio makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara za Mijini na Vijijini ambapo zaidi ya kilomita 846 za barabara zinaendelea kujengwa Unguja na Pemba kwenye mtandao wa barabara wenye takribani kilometa 1,344”, amesema Dkt. Mohamed.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!