Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya RAS Songwe ashangaa ujenzi zahanati kukwama kwa miaka miaka 4
Afya

RAS Songwe ashangaa ujenzi zahanati kukwama kwa miaka miaka 4

Spread the love

Katibu tawala mkoani Songwe, Happiness Seneda ametoa siku saba kwa uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe kupitia idara ya Afya kuanza ukamilishaji wa ujenzi wa baadhi ya majengo kwenye Zahanati ya Msia ambao ujenzi wake ulisimama baada ya fundi kukimbia. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Seneda ametoa maagizo hay oleo Jumatatu alipofanya ukaguzi kwenye zahanati hiyo na kubaini kusuasua kwa ujenzi huo unaotegemewa na wananchi.

Amewataka viongozi wa halmashauri ya Mbozi kukaa na wasimamizi wa idara ya afya wanaosimamia mradi huo kuona mapungufu yaliyopo na kuyafanyia kazi ndani ya siku saba ujenzi uanze.

“Haiwezekani ujenzi uanze mwaka 2019 hadi leo 2023 usikamilike ilihali ujenzi wenyewe baadhi ya sehemu hauridhishi, Serikali ilitoa fedha za ujenzi kitendo cha mradi kusua hakikubaliki,” amesema Seneda.

Awali akizungumzia hali hiyo Mganga mfawidhi wa zahanati hiyo, Amanyisye Rungwe amesema zahanati ya Msia iliyopo kijiji cha Msia, Kata ya Msia, tarehe 4 Oktoba 2021 walipokea fedha  kiasi cha Sh milioni 38 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji na usafi.

Amesema lengo la mradi ni kuongeza ufanisi wa huduma za afya ili kutoa huduma za matibabu na huduma za afya ya uzazi na mtoto, matundu sita na bafu moja na choo cha walemavu na watumishi vimejengwa.

“Baada ya kupokea maelekezo na taratibu za matumizi ya fedha hizo, shughuli za utekelezaji wa ujenzi zilianza rasmi Disemba 2021 ambapo shughuli za uchimbaji wa mashimo na chumba cha kujifungulia zilianza lakini ujenzi huo ulikwama baada ya mkandarasi kukimbia,” amesema.

Amesema baada ya mkandarasi kususia mradi walitafuta fundi mwingine ambaye alikuja na kupiga hesabu za gharama ya ujenzi hivyo wiki ijayo ataanza ujenzi.

Hata hivvyo, aliomba idaraya manununuzi waharakishe madokezo ya malipo ili waende kasi.

Mwenyekiti wa CCM kata ya Msia, Jiva Mwasenga amesema kitendo cha kusuasua mradi huo kimewaumiza wakazi wa kata hiyo hivyo ujio wa katibu tawala huyo umeleta tija.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mbunge ataka huduma Ultrasound itolewe bure kwa wajawazito

Spread the loveMBUNGE wa Viti Maalum, Esther Malleko, ameitaka Serikali kutoa bure...

Afya

Vituo 13 vyasitishiwa mkataba madai kutaka kupiga bilioni 4 za NHIF

Spread the loveVITUO vya kutoa huduma za afya 13, vimesitishiwa mikataba ya...

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

AfyaHabari za Siasa

Vifo vitokanavyo na UKIMWI vyapungua

Spread the loveVIFO vinavyosababishwa na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI), vimepungua kutoka...

error: Content is protected !!