Sunday , 12 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Dar: Chanzo ajali ya moto Kariakoo ni hujuma
Habari MchanganyikoTangulizi

RC Dar: Chanzo ajali ya moto Kariakoo ni hujuma

Spread the love

CHANZO cha ajali ya moto ulioteketekeza Soko la Kariako eneo la Mnadani na kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara zaidi ya 550, kimetajwa kuwa ni hujuma za baadhi ya wafanyabiashara. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Oktoba 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akitaja matokeo ya uchunguzi uliofanywa na kamati aliyounda kuchunguza chanzo cha tukio hilo lililotokea tarehe 1 Oktoba mwaka huu.

“Kamati imebaini kwamba moto huo haikuwa ajali bali ilikuwa ni hujuma ndani ya wafanyabiashara wenyewe na moto ulianzia katika eneo la mnadani. Maelezo haya yote yamebainika katika baadhi ya kamera za CCTV ambazo zilikuwa pembezeno wakati moto unaanza taratibu kabla haujaingia maeneo mengine,” amesema Chalamila.

Chalamila amesema “awali wafanyabiashara walisema umesababishwa na jenereta ambalo lilikuwepo pembezoni mwa maeneo hayo, lakini uchunguzi umebaini ni zima na linafanya kazi. Halikuungua wala hakikuwa chanzo cha moto huo.”

Hata hivyo, Chalamila hakuweka bayana namna hujuma hizo zilivyofanyika na kusababisha tukio hilo.

Chalamila ameagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini watu wanaodaiwa kuchoma moto soko la Kariakoo.

“Navielekeza vyombo vyote sasa vinavyoshughulika na masuala yanayohusiana na uvunjifu wa sheria viweze kuanza kazi yake mara moja kubaini watu waliofanya hivyo na kusababisha hasara.”

Akielezea namna kamati hiyo ilivyofanya uchunguzi wake, Chalamila amesema walichunguza eneo la tukio pamoja na kufanya mahojiano na baadhi ya mashuhuda, wafanyabiashara, wamiliki na walinzi wlaiokuwa zamu wakati tukio linatokea.

Mkuu huyo wa Dar es Salaam amesema kamati imetoa mapendekezo kadhaa kufuatia tukio hilo, ikiwemo halmashauri ya jiji hilo kuzingatia sheria ya upangaji majengo kwa kuweka njia za dharura ili kuweza kushughulikia matukio kama hayo kirahisi.

Pia imeshauri wafanyabiashara waliokuwa katika eneo hilo watafutiwe eneo lingine, pamoja na uchunguzi ufanyike kujua wamiliki halali wa biashara zilizoathirika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!