Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ASA yaongeza uzalishaji mbegu kufikia tani 3,500
Habari Mchanganyiko

ASA yaongeza uzalishaji mbegu kufikia tani 3,500

Spread the love

WAKALA wa Mbegu za Kilimo nchini (ASA), umesema uzalishaji mbegu imeongezeka kutoka tani 500 hadi kufikia 3,500. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Ongezeko hilo limetajwa leo Jumatano na Mtendaji Mkuu wa ASA Dk. Sophia Kashenge, akizungumza uwekezaji katika sekta hiyo uliofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, tangu alivyoingia madarakani miaka miwili na nusu iliyopita.

“Tunampongeza sana Rais Samia kwa kuongeza bajeti ya ASA iliyotuwezesha kuongeza uzalishaji mbegu kwa kiasi kikubwa,” amesema Dk. Kashenge.

Dk. Kashenge amesema ongezeko hilo linawasaidia wakulima Kupata mbegu bora kwa bei nafuu na kwa uhakika.


Amesema idadi ya mashamba ya ASA imeongezeka kutoka nane hadi 16, yaliyoko Tanzania Bara, ambayo kwa sasa yanayotumika ni asilimia 90.

Dk. Kashenge amesema uwekezaji wa miundombinu Katima shamba la mbegu lililoko eneo la Kilimo, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, utazalisha mbegu mara mbili mwaka ujao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!