Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Hima yajitosa mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia
Habari Mchanganyiko

Hima yajitosa mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia

Mkurugenzi wa Hima Organization Tanzania, Francisca Mawalla
Spread the love

 

SHIRIKA la Hima Organization Tanzania, limeanza kutoa mafunzo kwa makundi mbalimbali, juu ya namna ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mafunzo hayo ya siku moja yamefanyika leo tarehe 19 Septemba 2023, maeneo ya Kunduchi Mtongani, mkoani Dar es Salaam.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Hima Organization Tanzania, Francisca Mawalla,amesema wameanzisha ili kusaidia harakati za kupambana na rushwa ya ngono, ukatili wa kijinsia na kiuchumi.

“Tuko hapa kupambana na ukatili wa kijinsia, rushwa ya ngono na kutoa elimu ya kiuchumi na ujasiriamali, tumeanzisha shirika hili baada ya kuona uhitaji mkubwa wa kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia , hivyo tutawasaidia wahanga wakipata changamoto ili wajue wapi pa kuzipelekea na kupata majibu,” amesema Mawalla.

Diwani wa Kata ya Kunduchi, Michale Urio, alilitaka shirika hilo kutoa elimu kwa makundi yote hususan watoto ili waweze kuripoti wanaofanya vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi yao katika mamlaka husika.

“Mfano sasa hivi darasa la saba wamemaliza shule, hili ni jukumu lenu nawapa muandae kongamano mkawape elimu ya ukatili wa kijinsia ili watakapopangiwa shule katika maeneo mbalimbali wawe na uelewa juu ya suala hilo na kujua namna ya kujilindi,” amesema Urio.

Naye Afisa Maendeleo wa Kata ya Kunduchi,Theresia Kimario, amewataka wazazi na walezi kuwa karibu na watoto wao ili wapate kujua masuala yanayowasibu kwani baadhi yao hushindwa kuwasilisha vitendo vya ukatili wa kijinsia wanavyofanyiwa, kutokana na wao kukosa muda.

“Unakuta mtoto anakuja kwa mzazi anamuelezea shida zake, mzazi anamfukuza toka bila kumsikiliza. Wapo watoto wanapitia mazingira magumu tunapaswa kuwasikia ili tuwasaidie kabla hawajaharibika,” amesema Kimario.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!