Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Wanasiasa tusiburuze wananchi mchakato wa katiba mpya
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Wanasiasa tusiburuze wananchi mchakato wa katiba mpya

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amevitaka vyama vya siasa kutohodhi mchakato wa marekebisho ya katiba, akisema suala hilo si mali yao bali ni mali ya wananchi wote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akifungua mkutano maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa, leo tarehe 11 Septemba 2023, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amewataka wanasiasa kutowaburuza wananchi kuhusu mabadiliko ya katiba.

Mkuu huyo wa nchi, amesema mchakato huo utaanza na utoaji elimu kwa wananchi ili waielewe katiba, kwa kuwa asilimia kubwa hasa walioko vijijini hawaijui vyema.

“Tunaanza na elimu ya katiba, watanzania wajue ni kitu gani, wajue kinasemaje na kina nini sababu tunakokwenda viongozi wa kisiasa tunadhani tuna haki ya kuburuza watu.

Tunachokisema sisi watu wote wafanye hivyo. Katiba si kitabu ni morality ethical standard, tutaenda kwa mwendo huu kila mtu ajue,”amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema “tuna kazi kubwa ya kuwafanya watanzania waijue katiba ni nini na hiko kitabu kimekaaje. Wengine hawakijui ukienda huko vijijini mtu anaweza akaja na Ilani ya CCM akakwambia katiba, hajui ilani inasemaje wala katiba inasemaje hawajui.”

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema kamati maalumu itaanzishwa kwa ajili ya kusimamia mchakato huo, ambapo vyama vya siasa vitatoa uwakilishi wake.

“Tusiwaburuze, katiba viongozi wa siasa si yetu ni mali ya watanzania. Mwisho wa mkutano huu nimemwambia msajili nataka viongozi wa vyama walete maoni yao kwenye kamati itakayokwenda kuanzisha mchakato wa katiba na ninyi mtakuwa na wawakilishi wenu sio kila mtu ataingia kule,” amesema Rais Samia.

Msimamo wa Rais Samia kuanza kutoa elimu kwa wananchi juu ya katiba, umepinga vikali na baadhi ya makundi ikiwemo asasi za kiraia, ambayo yameshauri mchakato huo uanze moja kwa moja katika marekebisho kwa madai kuwa elimu ilishatolewa hapo awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!