Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu aonya Watanzania kufanya kazi badala ya kutegemea misaada
Habari Mchanganyiko

Askofu aonya Watanzania kufanya kazi badala ya kutegemea misaada

Askofu Dk. Benson Rutta
Spread the love

ASKOFU Mkuu wa kanisa la Glory to God Ministry for All Nations lenye makao makuu Mailimbili Jijini Dodoma, Dk. Benson Rutta amewataka watanzania kuhakikisha wanalinda amani pamoja na kujibidisha katika kufanya kazi badala ya kutegemea misaada. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waumini wa kanisa hilo leo tarehe 9 Septemba 2023 katika ibada maalumu ya kuliombea Taifa.

Askofu mkuu huyo amesema watanzania wana kila sababu ya kuhakikisha wanailinda amani ya nchi pamoja na kuhakisha wanafanya kazi kwa nia ya kujipatia kipato badala ya kuendelea kutegemea misaada.

Katika hatua nyingine kiongozi huyo wa kiroho amesema ili nchi iendelee kuwa na ustawi ni lazima rasilimali za nchi zilindwe kwa nia ya kuendeleza kizazi kijacho.

Kiongozi huyo amesema ili nchi iwe na maendeleo inatakiwa kuwa na watu ambao wana hofu ya Mungu kwa kuhakikisha wanasimamia haki pamoja na kulinda rasilimali za taifa bila kujinufaisha wao wenyewe.

Askofu Dk.Rutta ambaye alikuwa ni kiongozi katika kanisa la Full Gospel Bible Fellowship linaloongozwa na askofu mkuu Zacharia Kakobe na kujiengua kisha kuanzisha huduma yake inayojulikana kwa jina la Glory to God Ministry for All Nations, amesema kazi kubwa ya watumishi wa Mungu ni kuhakikisha wanasimamia ukweli ambao utalifanya taifa kuwa na neema wala siyo hiana.

Mbali na hilo Askofu Rutta amesema ili taifa liwe na ustawi linatakiwa kuwa na watu wenye hofu ya Mungu kwa kusimamia haki na wajibu pamoja na kutopenda kuwaonea watu wanaosimamia ukweli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!