Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa ampa Biteko mfupa ulioshinda Makamba, atoa siku 7
Habari za SiasaTangulizi

Majaliwa ampa Biteko mfupa ulioshinda Makamba, atoa siku 7

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amemuagiza Naibu wake, Dotto Biteko, kutafuta muarobaini wa changamoto ya uhaba wa mafuta ndani ya siku saba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waziri Majaliwa ametoa agizo hilo bungeni jijini Dodoma, akimjibu Mbunge wa Mlalo, Rashid Shangazi, aliyehoji hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha mafuta yanapatikana nchini wakati wote na kwa gharama nafuu.

Katika agizo lake hilo, Waziri Majaliwa alimtaka Biteko ambaye pia ni Waziri wa Nishati, kufanya kikao na taasisi zinazoshughulika na biashara ya mafuta, pamoja na wafanyabiashara, kuona namna ya kupanua wigo wa uagizaji wake, ili nchi iwe na akiba ya kutosha.

“Ili watanzania wapate huduma hiyo muhimu ya upatikanaji wa mafuta, wanunuaji na taasisi ya uuzaji wa mafuta mtengeneze kikao kikubwa na wizara zinazohusika. Mkae muone namna ya upatikanaji wa mafuta.

Naibu Waziri Mkuu, Dotto Biteko

“Tupanue wigo wa waagizaji mafuta ili tuwe na mafuta mengi nchini kwa usalama wa taifa letu na kama hii itafanyika ndani ya wiki moja tutakuwa tumepata majibu na tutawapa taarifa watanzania na naibu waziri mkuu atashughulikia hilo,” amesema Majaliwa.

Aidha, Waziri Majaliwa amesema Biteko ameshaanza kufanya vikao kadhaa na wadau kwa ajili ya kutafuta suluhu ya changamoto hiyo, iliyokuwepo tangu January Makamba, alivyokuwa Waziri wa Nishati.

“Kufuatia mabadiliko ya Rais Samia Suluhu Hassa aliyoyafanya juzi, tumeanza kumuona naibu waziri mkuu akifanya vikao kadhaa na wizara na kukutana na wadau. Kwa kuwa ameshaanza hii kazi niendelee kumuagiza kushughulikia suala hili zaidi mafuta yapatikane nchini, suala la bei tunajua zinabadilika wakati wote,” amesema Waziri Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!