Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wakili Mwabukusi mbaroni, yumo pia Masonga na Mdude
Habari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi mbaroni, yumo pia Masonga na Mdude

Spread the love

MWANASHERIA mahiri nchini na Wakili wa kujitegemea, Boniface Mwabukusi amekamatwa na jeshi la Polisi. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali, akiwamo Askofu Emmaus Mwamakula zinasema, Mwabukusi amekamatwa katika maeneo ya Mikumi, mkoani Morogoro. Anatuhumiwa kwa uchochezi.

Mwabukusi alikuwa mmoja wa wanasheria waliofungua kesi ya kupinga mkataba uliofungwa kati ya serikali na Dubai.

Mdude Nyagali

 Kukamatwa kwa Mwabukusi  kumekuja muda mfupi baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi kuutangazia ulimwengu, kwamba “kuna njama za kumuangusha Rais wa Jamhuri, Dk. Samia Suluhu Hassan.”

Akiandika kupitia mtandao wake wa kijamii, Askofu Mwamakula anasema,

“Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa wakili msomi Boniface Kanjunjule Mwabukusi, amekamatwa na Jeshi la Polisi kule Mikumi, Morogoro akiwa pamoja na Katibu wa Kanda wa CHADEMA, Emmanuel Masonga.

“Walikuwa safarini kuelekea Dar es Salaam pamoja na Mdude ndipo wakazuiwa Mikumi.

“Alikamatwa Mdude saa 10 usiku na baadaye maelekezo yakaja ya kukamatwa na wao pia. Mwabukusi ametujulisha kwa simu kuwa wao wameelezwa wamekamatwa kwa tuhuma za uchochezi na simu zao zimechukuliwa.

“Wakili Mwabukusi ndiye aliyesimamia kesi ya kupinga mkataba wa Bandari iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!