Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mgogoro wa ardhi wakwamisha ujenzi nyumba ya walimu Ileje
Elimu

Mgogoro wa ardhi wakwamisha ujenzi nyumba ya walimu Ileje

Spread the love

MGOGORO wa mpaka kati ya vijiji vya Sange na Mswima kata ya Sange wilayani Ileje mkoani Songwe umetajwa kukwamisha ujenzi wa nyumba ya walimu yenye thamani ya Sh 100 milioni. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe …(endelea).

Kusimama kwa ujenzi huo kulitokana na wananchi wa Kijiji cha Mswima kudai eneo inapojengwa nyumba hiyo ni eneo la Kijiji chao huku wananchi wa Kijiji cha Sange wakidai ni eneo halali la shule tangu ilipoanza.

Kitendo cha kushindwa kutatuliwa kwa mgogoro huo kimesababisa mradi huo kusimama licha ya fedha Sh mbili milioni kutumika kujenga msingi.

Kutokana na mzozo huo jana tarehe 17 Julai 2023 Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo kupitia kwa Mwenyekiti wake, Patrick Ghambi walipotembelea eneo hilo waliagiza nyumba hiyo ijengwe kwa kuwa ni eneo halali la shule na limeshapimwa.

Ghambi alisema maamuzi ya kuhamishwa eneo ambalo awali palijengwa msingi yatakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za serikali.

Alisema hakuna sababu za msingi kwa wananchi wa vijiji hivyo kugombea eneo la shule.

“Nawashangaa sana wananchi wa Mswima ambao ndio waanzilishi wa mgogoro huu. Ni eneno ambalo wananchi wengi wamesoma shule ya msingi Sange na wanajua mipaka ya shule…kwanini mlete migogoro ambayo haina tija?” alihoji Ghambi.

Ghambi alisema viongozi kuanzia ngazi ya vijiji mpaka wilaya wahakikishen wanaweka alama za mipaka ya taasisi ili kuepusha migogoro ambayo imezuia kuendelea kwa ujenzi wa nyumba ya walimu.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Ileje na mjumbe wa kamati ya siasa, Ubatizo Songa alisema wilaya walitenga zaidi ya sH 20 milioni  kwa ajili ya kupima maeneo yote ya taasisi ikiwepo na shule ya msingi Sange.

Alisema eneo hilo lipo kisheria kwani elimu haina mpaka hivyo ujenzi uendelee kama kawaida watakaoendelea kukwamisha watawajibishwa.

Mwenyekiti wa shule ya msingi Sange, Zawadi Kabuje alisema mgogoro huo unahusishwa na mvutano wa kisiasa hali ambayo imechelewesha mradi ambao ulipaswa kukamilika tangu tarehe 30 Juni mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Waziri SMZ akoshwa na kazi za Global Education Link

Spread the loveSERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar SMZ imesema itaendesha msako na kuzifutia...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

error: Content is protected !!