Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi yaanza uchunguzi tukio la kifo Mbezi Luis
Habari Mchanganyiko

Polisi yaanza uchunguzi tukio la kifo Mbezi Luis

Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeanza uchunguzi wa tukio la kifo cha Felix Mgeni, anayedaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum linachunguza tukio la kifo cha Mgeni (47), mkazi wa Kimara Temboni, anayedaiwa kuuawa huko maeneo ya Mbezi Luis usiku wa tarehe 14 Julai 2023. Mwili wa marehemu umekutwa kwenye gari aina ya Toyota Rav 4, huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani,” amesema Kamanda Muliro.

Kamanda Muliro amesema uchunguzi unaofanyika ni pamoja na, kupeleleza baadhi ya vitu vilivyokutwa eneo la tukio, vingine vikiwa ni vya jinsia ya kike.

“Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Mloganzila kwa uchunguzi zaidi na hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa baada ya uchunguzi wa kina,” amesema Kamanda Muliro.,

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!